Broadways Yatangaza Bei Mpya ya Mkate Kuanzia Julai 1, Wakenya Kulipa Zaidi

Broadways Yatangaza Bei Mpya ya Mkate Kuanzia Julai 1, Wakenya Kulipa Zaidi

  • Data za Shirika la Takwimu Nchini (KNBS) zilionyesha kuwa mfumuko wa bei Kenya, ulifikia 7.9% mwezi wa Juni kutokana na ongezeko la gharama ya chakula na mafuta
  • Wafanyabiashara walionya kuwa ongezeko la bei ya mafuta lililotangazwa Juni 30, lingesababisha bei za bidhaa kupanda kutokana na kuongezeka kwa gharama za uzalishaji
  • Kampuni ya Broadway ilirekebisha bei za mkate kuanzia Jumamosi, Julai 1, ili kusawazisha ongezeko la gharama za uzalishaji

MAKINIKA: Tusaidie kubadilisha maisha ya wengi, jiunge na programu ya Patreon kutoka TUKO.co.ke.

Wakenya watalazimika kulipa KSh 10 zaidi kununua mkate wa Broadways wenye uzito wa gramu 400.

Broadways Yatangaza Bei Mpya ya Mkate Kuanzia Julai 1, Wakenya Kulipa Zaidi
Mkate uliokatwa wa Broadways wenye uzito wa gramu 400 utauzwa kwa KSh 65. Picha: Bakery ya Broadway.
Chanzo: Facebook

Kampuni ya Broadway ilianza kurekebisha bei kuanzia Jumamosi, Julai 1, 2023.

Bei mpya za mkate

Kwenye mabadiliko ya bei ya Broadways, mkate wa premium wenye uzito wa gramu 400, ambao unanunuliwa sana na Wakenya, utauzwa kwa KSh 70, tofauti na KSh 60 awali.

MAKINIKA: Bofya “Ona Kwanza” chini ya “Fuatilia” ili kuona Habari za TUKO kwenye jukwaa lako la Habari

Pia soma

Kuanzia De Gea, Lingard Hadi Zaha: Wachezaji 10 Nyota wa EPL Ambao Sasa Hawana Klabu za Kuchezea

Mkate wa gramu 600 ambao ulikuwa unauzwa kwa KSh 80 sasa utauzwa kwa KSh 97, huku ule wa gramu 800 ukiuzwa kwa KSh 130.

Mkate wa Kadogo wa Broadways sasa utauzwa kwa KSh 32.

Mwezi wa Mei 2023, watengenezaji wa mkate walieleza kuwa gharama kubwa ya malighafi na uzalishaji ingewalazimisha kuongeza bei za mkate kwa hadi KSh 10.

Katika Kaunti ya Homa Bay, TUKO.co.ke iligundua kuwa mkate wa gramu 400 ulikuwa unauzwa kwa KSh 65 badala ya KSh 60, huku ule wa gramu 800 ukiuzwa kwa KSh 130 badala ya KSh 120.

Chanzo: TUKO.co.ke

Vichwa:
Online view pixel