Jinsi ya kupika mkate laini.

soft bread

Vifaa:

  1. Unga mweupe wa ngano – vikombe 3
  2. Sukari – 1/3 mug
  3. Maji – 3/4 Mug
  4. Maziwa ya unga – 1/2 mug
  5. Mafuta ya kula – 1/4 mug
  6. Mtindi – kijiko kimoja cha chakula
  7. Hamira ( instant) – viijiko 2 vya chakula
  8. Mayai – 1
  9. Hiliki.

Namna ya kupika:

  1. Koroga maziwa ya unga na maji
  2. Menya hiliki na uziponde.
  3. Kama unatumia hamira ya chenga weka katika kikombe kidogo, tia na sukari na maji iumke (weka pembeni)
  4. Kama unatumia  hamira ya unga (instant) changanya na unga moja kwa moja
  5. Chukua unga, weka amira iliyoumuka au instant, weka hiliki, halafu kanda mpaka unga uwe laini.
  6. Unga ukilainika ufunike kwa muda mpaka uumuke.
  7. Pakaza siagi katika kifaa (trey) utachotumia kuokea.
  8. Chukua mchanganyiko na uukate kwa size ya madonge upendayo, kisha weka katika trey ya kuokea.
  9. Kabla hujaweka kwenye oven, funika trey yenye madonge kwa muda ili yaumuke.
  10. Weka katika Oven yenye nyuzi joto 150 kwa dakika 15 mpaka igeuke rangi ya brown.
  11. Ikiiva toa kwenye oven kwa ajili ya kula.

 

Leave a comment